
Albert Chalamila, aliyekuwa Mkuu wa mkoa wa Mwanza
Taarifa ya utenguzi huo imetolewa usiku wa kuamkia leo Juni 11, 2021, na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Jaffar Haniu, zikiwa zimepita siku chache tu tangu Chalamila ateuliwa kuwa Mkuu wa mkoa huo akitokea mkoani Mbeya.
Aidha, Rais Samia amemteua aliyekuwa Mkuu wa mkoa wa Tabora Ally Hapi kuwa Mkuu wa mkoa wa Mara akichukua nafasi ya Mhandisi, Robert Gabriel Luhumbi, aliyehamishiwa mkoani Mwanza.
Sanjari na hayo Rais Samia pia amemteua, Batlida Buriani, kuwa Mkuu wa mkoa wa Tabora, kabla ya uteuzi huo Batlida alikuwa ni Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga.